
Xi Jinping amechaguliwa tena kuwa katibu wa chama kwa muhula wa tatu mfululizo katika historia ya nchi hiyo.
Putin alimwambia Xi kuwa anatarajia kuendeleza zaidi "uhusiano wa kina" kati ya nchi hizo mbili.
Washirika hao walikutana mara ya mwisho katika mkutano wa kilele wa Shirika la Ushirikiano wa Shanghai nchini Kazakhstan ambapo walifanya mkutano wa moja kwa moja kuthibitisha uhusiano wao.
Mwezi Februari nchi hizo mbili zilitangaza urafiki usio na "mipaka" na "hakuna maeneo yaliyokatazwa ya ushirikiano" muda mfupi kabla ya Urusi kuivamia Ukraine.