
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) Levocatus Mshumbusi,
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI) Levocatus Mshumbusi, wakati wakiendesha kikao kazi na watalaam wa tiba za asili mkoani Tabora na kusisitiza kuwa miti ya dawa katika misitu kwa sasa ipo kwa 25% tu ukilinganisha na ukubwa wa mahitaji .
Amesema ukiachilia mbali na shughuli zingine za kibinadamu kama kilimo ambazo zimekuwa ni sababu ya kuteketea kwa miti dawa, pia kumekuwepo na aina ya uvunaji mbaya wa kuua miti kabisa kwa kubandua magome na kuchimbua kwa kukata mizizi yake.
Aidha ametaja kuna kila sababu ya kuwekwa mazingira ya uhifadhi wa miti dawa kutokana na umuhimu wake wa kutumika kama dawa kwa faida sasa na vizazi vijavyo.