Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Majahazi yenye shehena za mafuta ya kula yakamatwa

Thursday , 8th Dec , 2022

Jeshi la Polisi Kikosi cha Wanamaji  Dar es Salaam, wamekamata majahazi matatu yakiwa yamebeba shehena ya mafuta ya kupikia yakiwa kwenye madumu ya lita 20 yapatayo 1231, yakitokea Zanzibar kuelekea Bandari bubu Kunduchi.

Moja ya Jahazi lililokamatwa na shehena ya mafuta

Kamanda wa Kikosi cha Polisi Wanamaji ACP Moshi Sokoro, amebainisha kuwa walifanikiwa kukamata mafuta Desemba 6, 2022, nyakati za jioni maeneo ya Kunduchi, wilaya ya Kinondoni mkoa wa Dar es Salaam katika Bahari ya Hindi.

ACP Sokoro amefafanua kuwa Jahazi la kwanza litambulikalo kwa jina SV. Hudallah likiongozwa na nahodha Issa Bakari (26 ) mkazi wa Bububu Kihinani Zanzibar akiwa na wenzake 4, lilikutwa na madumu yapatayo 500 ya lita 20 aina ya Royal, Jahazi la pili SV. Wabaya si wote likiongozwa na nahodha Ramadhan Hamisi (42) mkazi wa Uzi Zanzibar akiwa na wenzake 3, likiwa na madumu 351 ya lita 20, Jahazi la 3 ni SV. Bora salama likiongozwa na Mwalimu Hamisi (40) mkazi wa Uzi Zanzibar akiwa na wenzake 2, likiwa na madumu 351.

Aidha kikosi hicho kiliendelea na operesheni na majira ya usiku wakafanikiwa kukamata majahazi mengine mawili, ambayo ni SV Thamarat likiongozwa na Ramadhani Eliasi (30), mkazi wa Mwanakwerekwe Zanzibar akiwa na wenzake 4 likiwa limebeba madumu 650, na Jahazi lingine SV. Subra Ngumu likiongozwa na nahodha Juma Shaibu (51) mkazi wa Mahonda Zanzibar, akiwa na wenzie 3, likiwa limebeba madumu 500, hivyo kufanya jumla ya madumu ya mafuta yaliyokamatwa kuwa 2381.

Aidha upelelezi wa awali umeonyesha kuwa mzigo huo ulitakiwa kushuka katika bandari ya Mbweni ambapo taratibu za kulipa ushuru wa forodha zingekamilika na badala yake watuhumiwa hao walielekea katika bandari bubu ya Kunduchi ili kushusha mizigo hiyo.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa