Thursday , 8th Dec , 2022

Zimebakia siku mbili kabla ya hatua ya Robo Failani kutimua vumbi nchini Qatar, hizi ni rekodi mbalimbali za timu zitakazopambana kwenye hatua hiyo kuanzia Ijumaa, Disemba 9, 2022.

Mastaa wa timu zilizofuzu hatua ya Robo Fainali Kombe la Dunia 2022

England itapambana na Ufaransa, timu hizi zitakutana kwa mara ya 3 kwenye fainali za Kombe la Dunia ambapo kwenye michezo 2 iliyopita yote England ilishinda. Mwaka 1966 waliinyuka Ufaransa mabao 2-0 na 1982 walishinda mabao 3-1. Huu pia utakuwa mchezo wa 32 timu hizi zinakutana kwenye mashindano yote, England wameshinda mara 17 sare michezo 5 na Ufaransa wameshinda mara 9.

Argentina watapambana na Uholanzi, ambapo rekodi zinaonesha timu hizi zimekutana mara 5 kwenye Kombe la Dunia. Uholanzi wameshinda mara 2, Argentina wakishinda mara moja na mara 2 wakitoka sare. Mara ya mwisho timu hizi kukutana kwenye Kombe la Dunia ilikuwa mwaka 2014 hatua ya Nusu Fainali nchini Brazil ambapo Argentina ilishinda kwa mikwaju ya penati 4-2.

Mchezo mwingine ni Croatia dhidi ya Brazil. Croatia hawajawahi kuifunga Brazil kwenye michezo minne waliyokutana. Wamefungwa mara 3 na wametoka sare mchezo mmoja, Neymar Jr ndiye mchezaji wa Brazil anayeongoza kuifunga Croatia akiwafunga mabao matatu.