
Mahakama ilimtia hatiani kwa shtaka la "uadui dhidi ya Mungu" baada ya kubaini kuwa aliwachoma kisu hadi kuwaua wanachama wawili wa kikosi cha kijeshi cha Basij Resistance Force.
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameonya kuwa waandamanaji wanahukumiwa kifo kutokana na kesi zisizofuata taratibu.
Mauaji ya kwanza kuhusiana na machafuko hayo yalifanyika siku ya Alhamisi wiki iliyopita, na kusababisha shutuma za kimataifa.
Mohsen Shekari, mwenye umri wa miaka 23, alipatikana na hatia ya "uadui dhidi ya Mungu" baada ya kupatikana amemshambulia mwanachama wa Basij kwa panga katika mji mkuu, Tehran.