Ruto ambaye alitangazwa mshindi katika uchaguzi huo amesema njama hizo zilipangwa baada ya kumalizika uchaguzi na kabla matokeo hayajatangazwa
"Tunajua kuwa kulikuwa na jaribio la moja kwa moja la kumteka nyara Bw Chebukati na kumuua ili tume isiweze kutekeleza kazi yake, au kamishna aliyetii sheria achukue mamlaka na kupotosha mamlaka ya watu. Ilikuwa wakati mgumu, baridi na upweke, vitisho vilikuwa vikali., zawadi zilizoahidiwa ni nyingi na shinikizo lisilokoma,” Rais Ruto alisema.
Aidha aliyekuwa mpinzani wake katika uchaguzi huo Raila Odinga, amesema tuhuma hizo hazina ukweli huku akitaka madai hayo yawasilishwe kwenye jopo la uchunguzi ili ukweli ujulikane
