Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga kuondoka Machi 30,2023

Wednesday , 22nd Mar , 2023

Kikosi cha klabu ya Yanga kinataraji kuondoka nchini Jumanne ya Machi 30 kuelekea nchini DR Congo kwa ajili ya mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya TP Mazembe utakaochezwa Jumapili Aprili 2, 2023.

Afisa Habari wa klabu ya Yanga, Ali Kamwe amesema wanaendelea na maandalizi ya safari hiyo lakini amesisitiza licha ya kwamba wameshatinga robo fainali ya michuano hiyo lakini bado wanauhitaji ushindi dhidi ya TP Mazembe mabingwa wa zamani wa kombe hilo.

"Tunajivunia kuwa na mashabiki bora kwenye Klabu na hili tumelidhibitisha kwenye michezo yetu mitatu ya Kimataifa tukiwa nyumbani na sasa Uongozi wa Klabu umeamua lazima usafiri na mashabiki wake kwenda nao Congo kwenye mchezo wetu wa mwisho kwenye hatua ya makundi"amesema Kamwe

Kwa upande mwingine:Ali Kamwe ametangaza kuwa kutakuwa na uratibu mzuri wa Usafiri kwa mashabiki, wanachama na wapenzi wa klabu hiyo kwa ajili ya kwenda nchini DR Congo kuutazama mchezo huo.

Vile vile Yanga SC imethibitsha kuwa itawakosa nyota wake watatu kwenye mchezo huo, Mlinda mlango Djigui Diarra, kiungo Khalid Aucho na beki Djuma Shabani ambao wanakosekana kwasababu za kikanuni baada ya kuoneshwa kadi za njano mfululizo.

Yanga SC ndiye kinara wa kundi D ikiwa na alama 10 sawa na US Monastir ya Tunisia ambao wanatofautiana kwa magoli ya kufunga na kufungwa, TP Mazember watatu akiwa na alama 3 huku AS Real Bamako ya Mali ikishika mkia ikiwa na alama 1.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton