Friday , 5th May , 2023

Mashirika ya kijasusi ya Ukraine yaliripoti wiki hii kwamba yalifichua mpango wa kusafirisha injini za ndege ya kijeshi ya An-74 kutoka Ukraine hadi Iran.wachunguzi wa Ukraine wanadai kwamba Iran imekuwa ikitumika kama nchi ya kati tu ilhali Urusi anaweza kuwa mnunuzi halisi.

Habari hii ilianza mwaka 2011, wakati shirika la ndege la Lviv Airlines lilifutiliwa mbali nchini Ukraine. Kisha mali zote za shirika hili la ndege zilipaswa kuhamishiwa kwenye mfuko wa mali ya serikali, lakini kulikuwa na usiri mkubwa hali ya kwamba serikali ilifichwa huku sehemu ya mali ya shirika hilo ikipelekwa katika mikoa mingine kwa uuzaji zaidi.

Vipuri vya ndege nchini Ukraini viko chini ya udhibiti wa mauzo ya nje, kwa hivyo haingewezekana kuviuza hivyo hivyo. Walipanga kuvificha na kuvitoa nje chini ya vipengele vya mabomba ya gesi kwa kutumia nyaraka za kughushi. Kwa hili, wanunuzi wa kigeni waliahidi kulipa $ 400,000 kwa kila injini.

Kulingana na vyanzo vya mamlaka ya uchunguzi, hii inaweza kuwa mpango wa magendo kwa ajili ya kusafirisha bidhaa za kijeshi kutoka Ukraine hadi Urusi kupitia nchi tatu. Kwa uwezekano wote, ununuzi huo ulikusudiwa kwa ndege za usafirishaji wa jeshi la Urusi.

D-36 ni injini ya ndege ya turbojet yenye mzunguko wa pande mbili, iliyozalishwa kwa wingi katika kiwanda cha Zaporizhzhya Motor Sich mnamo 1977 kwa ajili ya ndege ya Antonov.

An-74 ni muundo wa polar wa ndege ya usafirishaji ya An-72, ndege iliyofanikiwa sana ya usafirishaji na nyepesi iliyotengenezwa katika Ofisi ya Ubunifu ya Antonov miaka ya 1970. Kwa sababu ya kumiliki eneo lisilo la kawaida la injini juu ya ndege, ndege hii inaweza kutua kwenye njia ndogo,ambazo ni duni.