Sunday , 14th May , 2023

Kijana mmoja aitwaye Ahmed Abdallah mkazi wa kijiji cha Mapogolo kata ya Milo wilayani Ludewa mkoani Njombe, amekamatwa na polisi baada ya kugundulika kutoa huduma ya afya kwa miaka 18, kinyume cha sheria ikiwemo mazingira yasiyo salama na kutokuwa na vyeti vya taaluma hiyo.

Baadhi ya vifaa alivyokuwa anatumia kwenye kazi zake

Wakati wa mahojiano na Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Leslie Mhagama mtuhumiwa huyo amedai kuwa na elimu ya msalaba mwekundu huku akiomba kutotoa maelezo zaidi mpaka pale atakapofikishwa kituo cha polisi.

Unaweza kutazama video yote kwenye YouTube Channel ya East Africa TV hapo chini.