Thursday , 19th Mar , 2015

Star wa muziki King Crazy GK kutoka kundi la East Coast ameongea na eNewz kuhusu ujio wake mpya na kusema kuwa, kwa sasa amejipanga kuingiza sokoni muziki wa live, akiwa pia amejinoa vilivyo kwa upande wa kuimba na pia kupiga vyombo vya muziki.

msanii wa muziki wa bongofleva nchini KinG Crazy GK

GK amewataka mashabiki wake kufahamu kuwa, muda wote ambao amekuwa nje ya gemu ya muziki, amekuwa akijiongezea elimu kwa upande wa sekta hiyo, akijiamini kuwa aliacha muziki akiwa ngazi ya juu, na anarejea akiwa ngazi ya juu zaidi sambamba na ujuzi wa kitaalam katika fani hiyo.