Zverev aondolewa Mexican Open
Mchezaji namba 3 kwa ubora katika mchezo wa tenisi duniani na bingwa wa Olympic Alexander Zverev ameondolewa katika michuano ya Mexican Open baada ya kuipigiza raketi yake na kuigonga miguu ya mwamuzi huku akitoa lugha chafu za matusi akimlaumu msimamizi huyo kwamba ameharibu mchezo.

