Mtoto afungwa kwenye mfuko na kutumbukizwa chooni
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera, limefanikiwa kumuokoa kutoka ndani ya shimo la choo cha shule, mtoto mchanga wa kiume mwenye umri wa kati ya siku mbili hadi tatu aliyetupwa katika shimo hilo na mtu ambaye hajafahamika, akiwa amefungwa kwenye mfuko.