Uchaguzi Mkuu, anguko kwa wapinzani
Oktoba 28, 2020, Tanzania iliingia kwenye joto la uchaguzi, kwa wananchi wake kuwachagua viongozi wao wanaowataka kwa nafasi za kiti cha urais, ubunge, udiwani na wawakilishi kwa upande wa Zanzibar, ambapo kwa mujibu wa viongozi wa serikali walisema kuwa uchaguzi huo ulifanyiaka kwa amani.