CORONA: Hadithi ya mapambano isiyoisha utamu
Machi 16, 2020, Tanzania ilithibitisha kisa cha kwanza cha mgonjwa wa Corona, taarifa ambayo ilitolewa na Waziri wa Afya wa wakati huo Ummy Mwalimu, ambaye alisema kuwa mgonjwa ni mwanamke raia wa Tanzania aliyewasili nchini Machi 15 kupitia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanajaro.