Akizungumza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Wakili wa Serikali Wankyo Simon, amesema kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekwishakamilika na kwamba upo katika hatua za mwisho za uchapishwaji ili jalada hilo lipelekwe Mahakama Kuu.
Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mkuu wa Mahakama hiyo Salumu Ally, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 4, 2019.
Mshtakiwa huyo anadiwa kutenda kosa hilo Mei 15, 2019, nyumbani kwake maeneo ya Gezaulole Kigamboni.