Jumanne , 26th Dec , 2017

Mwenyekiti wa Wilaya ya Siha (CHADEMA), na Diwani wa Kata ya Gararagua ametangaza kujivua nafasi zake zote za uongozi ndani ya Chama hicho na kutangaza anahamia Chama Cha Mapinduzi kuungana na Rais Magufuli kulinda rasilimali za nchi.

Mwenyekiti Zakaria Lazaro Lukumay amesema kwamba anaamini kwamba CCM ndicho chama pekee ambacho kinagusa maisha ya watanzania hivyo ameamua kujiunga ili kutetea, kulinda, na kusimamia rasilimali za nchi ikiwa ni pamoja na kupiga vita ufisadi, rushwa na mambo mengine yanayofanana na hayo.

Katika taarifa yake aliyoituma kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha,  Lukumay ameongeza kuwa anaamini katika maamuzi yake aliyoyafanya atakuwa huru kuungana na Mh. Rais Magufuli katika kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015 .

Mtazame hapa chini Diwani Lukumay akifunguka zaidi