
Maagizo hayo yapo kupanda miti rafiki wa maji kwenye vyanzo na kushusha bei ya gesi ya kupikia ili wananchi waachane na matumizi ya mkaa ambao unachangia uharibifu wa mazingira
Dkt. Mpango ametoa maagizo hayo kwenye mkutano wa nane wa Mwaka Bodi za Maji za Mabonde unaofanyika kitaifa jijini Mbeya pamoja na uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti rafiki wa maji kwenye vyanzo.
Waziri wa Maji, Juma Aweso, amesema shughuli za kibinadamu kama vile kilimo, uchomaji mkaa zimechangia kwa kiasi kikubwa kuharibu vyanzo vya maji huku Spika wa Bunge la Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini, akibainisha haya.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, TAMISEMI, David Silinde amesema wakuu wa Mikoa yote nchini wanapaswa kuandaa mpango kazi wa upandaji miti rafiki wa vyanzo vya maji kwenye maeneo yao na taarifa hiyo wapatiwe.