Amesema kuwa kupitia kikosi hicho wamejipanga vyema kukabiliana na madawa ya kulevya pamoja na vilipuzi vya aina yeyote ile katika mkoa wa huo
Sambamba na hilo kamanda Masejo amesema kuwa Jeshi hilo kupitia kikosi cha mbwa na farasi kinatoa mafunzo kwa mbwa wa kirai ilikuimarisha ulinzi na usalama katika mkoa wa Arusha
Kwa upande wake mkuu wa kikosi cha Mbwa na farasi mkoa wa Arusha mrakibu msaidizi wa Polisi ASP William Mwaisumo amesema kuwa kikosi hicho kimejipanga vyema kutoa mafunzo kwa mbwa wote watao letwa kupata mafunzo ya ulinzi na utambuzi wa madawa vilipuzi.