Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Juma Homera
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Juma Homera, ndiye aliyetoa agizo hilo wakati wa maadhimisho ya siku ya Mashujaa iliyofanyika eneo walipozikwa mashujaa hao ambapo maofisa mbalimbali wa serikali waliweka mashada kwenye makaburi hayo.
Katibu Tawala mkoa wa Mbeya, Dk. Angelina Lutambi, amesema siku ya mashujaa nchini inatoa nafasi ya kuwakumbuka na kuwaombea watu mbalimbali waliopoteza maisha.
Viongozi wa dini na wananchi wa Jiji la Mbeya wakapongeza hatua ya serikali kujenga mnara utakotambulisha majina ya mashujaa 36 waliofariki wakilipigania Taifa na mataifa mengine.