Jumatatu , 4th Mei , 2020

Watoto wawili wamefariki Dunia kufuatia kuungua moto kwa nyumba waliyokuwa wakiishi, katika mtaa wa Makuburi Ubungo jijini Dar es salaam. 

Mshumaa

Akizungumza na EA Radio Mwenyekiti wa Mtaa Makuburi, Moshi Kaftany amesema chanzo cha moto inadaiwa ni mshumaa.

Kaftany amesema kuwa "moto umetokea usiku wa kuamkia leo na wajukuu zangu wawili wamefariki, bahati mbaya zaidi, hakuna hata mpangaji aliyefanikiwa kuokoa chochote"

Tazama video kamili hapo chini