Alhamisi , 3rd Mar , 2022

Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora linamshikilia kijana Michael Jacobo (25) mkazi wa Kijiji cha Upungu wilaya ya Nzega kwa tuhuma kumuua baba yake mzazi Jacobo Lubela, baada ya  kumvizia majira ya jioni akiwa nje ya  nyumba na kumkata shoka kichwani, shingoni  na mikono yote miwili.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao, amesema tukio hilo limetokana na  imani za kishirikina ambapo mtuhumiwa amekuwa akisumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa ambao amekuwa akiuhusisha kulogwa na baba yake  mzazi .

Kamanda Abwao amesema mtuhumiwa huyo baada ya kutiwa nguvuni alihojiwa na kukili kutekeleza mauaji hayo ambapo kwa sasa  zinafanyika taratibu za kumfikisha mahakamani.