Jumatatu , 1st Sep , 2025

"waliofariki katika mlipuko huo ni Dotto Mrisho (24) na Said Ramadhani (53) aliyejeruhiwa ni Hassan Omary mkazi wa Sanzale, Bagamoyo" Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase.

Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limethibitisha kutokea kwa tukio la watu wawili  kupoteza maisha  papo hapo na mmoja  kujeruhiwa vibaya mwilini baada ya kutokea kwa mlipuko unaodaiwa  kutokana na chuma ambacho mmoja wao alikua anakikata kwenye Banda  linalojihusisha uchomeleaji vyuma chakavu  huko Mtaa wa Magomeni Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase amesema tukio hilo limetokea jana Agosti 31  na kwamba mlipuko huo pia umeshababisha  uharibifu wa nyumba kadhaa zilizopo jirani na ilipotokea mlipuko huo. 

Amebainisha  Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina Kwa kushirikiana na vyombo vingine vya  usalama Ili kubaini chanzo Cha mlipuko huo na ni wa kitu gani kisha taarifa kamili itatolewa mapema iwezekanavyo.