
Ziara wilayani Chato
Katika ziara hiyo, Rais Museveni atamtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, Kijijini kwake Mlimani, wilayani Chato, mkoani Geita.
Akiwa kijijini hapo, Rais Museveni atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli. Ikumbukwe hivi karibuni Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta alimtembelea Rais Magufuli nyumbani kwake, ambapo alifanya mazungumzo naye binafsi.