Dkt. Philip Mpango - Waziri wa Fedha na Mipango
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizindua Bodi ya Shirika la Bima la Taifa NIC na kwamba hatua hiyo itaisaidia kutunza na kulinda mali za umma dhidi ya majanga na ajali.

Israel Kauzora - Kamishna wa Bima
Kamishna wa Bima nchini Bw. Israel Kamuzora amesema kwa muda mrefu jamii imekosa elimu juu ya umuhimu wa bima kwenye uchumi na kwamba kuanzia sasa watahakikisha elimu inayafikia makundi yote na hasa jinsi bima inavyoweza kuchochea uchumi na ukuaji wa biashara.

