Jumanne , 14th Mar , 2017

Bei ya nyanya katika masoko mbalimbali Jijini Dar es Salaam imepanda kilinganishwa na hali ilivyokuwa wiki mbili zilizopita ambapo kwa sasa bei ya jumla imepanda kutoka shilingi elfu 35 kwa sanduku na kufikia shilingi elfu 60.

Biashara ya Nyanya katika moja ya soko Dar es Salaam

Baadhi ya madalali wanaoshusha nyanya katika masoko mbalimbali wameiambia EATV kuwa bei imepanda kutokana na kiasi kidogo cha shehena ya nyanya kinachoingia sokoni hapo kwa sasa wanategemea nyanya kutoka kwa wakulima wa Arusha, Iringa na Makambako pekee.

Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wadogo wanaouza nyanya kupitia vipimo vya asili maarufu kama sado, wamesema kupanda kwa bei kumefanya biashara kuwa ngumu kwani wateja wamekuwa hawamudu ongezeko hilo la bei.