Ijumaa , 1st Jan , 2016

King of the Best Melody Christian Bella ametoa shukrani kwa vyombo vya habari na wadau wote katika sekta ya burudani nchini akiweka wazi pia mafanikio kupitia bendi yake ya Malaika Music band.

Staa wa muziki wa dansi nchini King of the Best Melody Christian Bella

Bella amesema mafanikio hayo ni pamoja na kazi zake zote zilizotamba mwaka 2015 ikiwemo kufanya kolabo na gwiji wa miondoko ya bolingo, Koffi Olomide.

Mkali huyo amesema kuwa kuanzia mwaka huu mpya amejipanga pia kuanzisha studio yake mpya akiweka wazi kuwa kila baada ya mwezi mmoja atakuwa akitoa nyimbo kali, hivyo mashabiki wawe tayari kupokea kazi mpya kutoka kwake.