
mwanamuziki wa Uganda Iryn Namubiru
Iryn ambaye amekuwa moja ya wasanii waliokuwa mstari wa mbele kupeleka ujumbe wa Faraja kwa Juliana, amewataka mashabiki wake kufahamu kuwa, uzinduzi wa video hii utafanyika katika tarehe ambayo ataitangaza baadaye baada ya msiba kumalizika.
Mwili wa marehemu Keron tayari umekwishafikishwa nchini Uganda jana ukilakiwa na umati mkubwa wa waombolezaji ambao pia walitarajia kumuona Juliana katika msafara huo na kumpatia pole bila mafanikio kutokana na msanii huyo kutoonekana kabisa.
