
Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa
Taarifa iliyotolewa na katibu mkuu wa Wizara hiyo Prof. Kitila Mkumbo imeeleza kuwa walioteuliwa ni Mhandisi Mbike Jones Lyimo ambaye atakuwa Mkurugenzi wa KUWASA mkoani Kigoma.
Mwingine ni Bi. Flaviana Kifizi, ambaye amekuwa mkurugenzi wa SHUWASA mkoa wa Shinyanga.
Wa tatu katika walioteuliwa ni Mhandisi Robert Lupoja ambaye anakuwa mkurugenzi wa MUWASA huko Musoma mkoani Mara.