Alhamisi , 16th Mei , 2019

Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa, leo Mei 16, 2019 amefanya uteuzi wa Wakurugenzi watendaji watatu wa mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira.

Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa

Taarifa iliyotolewa na katibu mkuu wa Wizara hiyo Prof. Kitila Mkumbo imeeleza kuwa walioteuliwa ni Mhandisi Mbike Jones Lyimo ambaye atakuwa Mkurugenzi wa KUWASA mkoani Kigoma.

Mwingine ni Bi. Flaviana Kifizi, ambaye amekuwa mkurugenzi wa SHUWASA mkoa wa Shinyanga.

Wa tatu katika walioteuliwa ni Mhandisi Robert Lupoja ambaye anakuwa mkurugenzi wa MUWASA huko Musoma mkoani Mara.