Jumanne , 29th Nov , 2022

Taasisi ya kupambana na kuzuia Rusha (TAKUKURU) Mkoa wa Rukwa imesema imepokea kesi 54 kati ya hizo taarifa 32 zinahusu rushwa kutoka katika taasisi mbalimbali za umma na binafsi katika kipindi cha miezi 3 ambao ni mwezi Julai hadi  Mwezi Septemba 2022 

Akitoa taarifa Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Rukwa Owen Jasson amesema tayari kesi 13 zinaendelea Katika mahakama mbalimbali za Mkoa wa Rukwa, ambapo kati ya hizo kesi mbili zilitolewa maamuzi na Jamhuri kusinda kesi zote

Aidha Katika hatua nyingine Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Rukwa amesema katika chaguzi mbalimbali za ndani ya Chama cha Mapinduzi zilizofanyika wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kuthibiti mianya ya Rushwa na kutoa wito kuhakikisha vitendo vya Rushwa vinakomeshwa Katika chaguzi.