Auawa kwa kukatwa mapanga na binamu yake
Mwanafunzi wa darasa la 7 shule ya msingi Mwenge manispaa ya Morogoro, Faidhati Ibrahim (13), ameuawa kwa kukatwa na mapanga na binamu yake Shomari Malima, akiwa nyumbani kwao mtaa wa Tambukareli, huku sababu ikitajwa ni ugomvi wa kifamilia kati ya mama wa marehemu na mama wa mtuhumiwa.

