Singida United yachekelea SportPesa Super Cup
Kocha msaidizi wa Singida United Fred Minziro amesema mashindano ya SportPesa Super Cup yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Juni 05 mwaka huu ni kipimo kizuri kwa timu yake kwa ajili ya maandalizi ya kuelekea katika msimu ujao wa ligi kuu.

