Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

UKAWA waanza mbio zao, elimu kipaumbele cha kwanza

Saturday , 29th Aug , 2015

Chama Cha Demokrasi na Maendeleo kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) leo kimezindua rasmi kampeni za urais ambapo uzinduzi huo umeshuhudia umati wa watu wakijitokeza.

Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA akiwakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA, Mh. Edward Lowassa

Akiongea katika mkutano huo Mgombea urais kupitia Umoja huo Mh. Edward Lowassa amesema kuwa wananchi watakapompa ridhaa ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ataendesha mchakamchaka wa mabadiliko katika sekta zote.

Mh. Lowassa amesema kuwa ataweka vipaumbele katika sekta ya viwanda pamoja na kuboresha sera ya elimu ambayo ndio chachu ya mabadiliko katika kujenga uchumi wa nchi yoyote duniani.

Kwa upande wake mgombea mwenza Juma Duni Haji amesema kuwa watanzania wametaabika kwa muda mrefu bila kupata utatuzi wa matatizo yao ikiwemo maisha bora ila kwa serikali itakayoundwa na Mh. Lowassa itajenga mazingira bora kwa kila mtanzania.

Naye waziri mkuu mstaafu wa awamu ya tatu Mh. Fredrick Sumaye amesema kuwa ufisadi unaofanyika ndani ya Chama cha Mapinduzi ni mkubwa na wao kwa nafasi zao walikuwa wanashindwa kufanya maamuzi kutokana na mfumo uliokuwepo ndani ya chama hicho.

Aidha Mh. Sumaye amefafanua kashfa zinazotokea nchini Tanzania nyingine ni mpango wa kutengeneza kuwachafua baadhi ya watu kwa kuwa chama hicho kina mgawanyiko mkubwa ambapo watu wenye msimamo wanachafuliwa ili wasipate nafasi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe amesema kuwa wamemchagua lowassa kuongoza mabadiliko kwa kuwa ni mtu ambae anauwezo wa kuamua na kuwatumikia wananchi.

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini