Waziri Ummy Mwalimu akikabidhi misaada kwa mkuu wa mkoa wa Kagera
Hatua hiyo inakuja hasa katika kipindi hiki ambacho mvua zimeanza kunyesha mkoani humo.
Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu wakati akikabidhi misaada ya Dawa, Vifaa kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko mkoani humo.
Akizungumza baada ya kupokea misaada hiyo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu amewaomba wadau wengine kuendelea kutoa misaada kwa ajili ya kurejesha hali ya kawaida baada ya maafa kutokea.