Thursday , 19th Mar , 2015

Burudani kali na aina yake kutoka mpambano mkali wa Masumbwi itachukua nafasi yake ndani ya Jiji la Dar katika ukumbi wa Diamond Jubilee, na kutoa nafasi kwa watu wote kushuhudia mapambano makali kabisa kuwahi kutokea ya ndondi.

pambano la ngumi la Word Title Eliminator litakaofanyika Dar es Salaam

Tukio hili la aina yake sambamba na burudani ya muziki litahusisha mapambano jukwaani ya mabondia kati ya Karama Nyilawila naThomas Mashali, Japhet Kaseba na Mada Maugo, Ashraf Suleiman na Joseph Rabotte toka USA na vilevile Pambano kubwa kabisa Machi 27 watakutana na Mohamed Matumla na Wang Xin Hua toka China.

Hii haijawahi kutokea popote pale, tunapotezea viwanja vingine vyote, mastaa na wadau mbalimbali wa burudani wote tunakutana pale Diamond Jubilee Machi 27 kuanzia saa moja kamili jioni, wenyewe wanasema #NiNgumiTu.