Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Niyonzima afunguka maumivu na alichoifanyia Simba

Tuesday , 19th Mar , 2019

Kiungo wa kimataifa wa Simba kutoka Rwanda, Haruna Niyonzima, ameweka wazi kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye mchezo dhidi ya AS Vita, aliumia kifundo cha mguu lakini hakutaka kutoka wala kuwaangusha mashabiki.

Haruna Niyonzima (katikati)

Niyonzima ambaye alifanya kazi kubwa ya kusaidia kupatikana kwa bao la ushindi la Simba ambalo liliwapeleka robo fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika, amesema siku zote alikuwa na ndoto hiyo hivyo hakutaka kuiacha.

''Niliumia lakini nikajiambia siruhusu hili linikwamishe, sikutaka kuwaangusha mashabiki na kocha kwa kuniamini ukizingatia nilifanya maandalizi ya muda mrefu kwaajili ya siku moja kufanya kitu kama hicho, hivyo nakiri Machi 16, 2019 ilikuwa siku yangu kubwa kwenye soka ngazi ya vilabu'', - Amesema Niyonzima.

Aidha amemshukuru kocha wake Patrick Aussems kwa kumwamini na kumpa dakika chache za kutimiza malengo yake. Niyonzima aliingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Emmanuel Okwi.

Niyonzima amemaliza kwa kusema kuwa baada ya kufika robo fainali sasa anaamini kuwa, wanayo nafasi ya kufika fainali na kikosi chao kinauwezo huo kwa kuzingatia wingi wa mashabiki walionao.

Simba imetinga hatua ya robo fainali Jumamosi Machi 16, 2019 baada ya kuifunga AS Vita mabao 2-1 na kufikisha alama 9 nyuma ya Al Ahly yenye pointi 10 kwenye kundi D. 

 

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao