
Mashabiki katika uwanja wa Taifa
Afisa Habari wa Simba SC Haji Manara amesema, kitendo kilichotokea katika mchezo dhidi ya Yanga siyo cha kiungwana na iwapo watagundua ndani ya vurugu hizo kutakuwa na mwanachama wa Simba basi watamchukulia hatua huku wakisema kuwa kwa sasa hawana mpango wa kutafuta Uwanja mbadala ya Uwanja wa Taifa mpaka serikali itakapotoa jibu kuhusu ombi lao la msamaha.
Simba imepigwa faini ya Sh milioni 5 kutokana na mashabiki wake kung’oa viti huku serikali ikivifungia vilabu vyote viwili vya Simba na Yanga kuutumia Uwanja huo kwa muda usiojulikana.