Stars ilijipatia ushindi huo kupitia mshambuliaji wake Elias Maguri kunako dakika ya 18 na kuifanya timu yake kujikatia tiketi ya moja kwa moja kuingia hatua ya nusu fainali ambapo itaenda kuminyana na Zambia siku ya Jumatano ya Julai 5 mwaka huu.
Kwa matokeo hayo mazuri Taifa Stars imeweza kurudisha imani kwa watanzania wapenda soka na endapo wataendelea kucheza kwa uwezo huu, basi kuna asilimia kubwa ya kuweza kufika hata kombe la dunia siku za usoni.




