Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waamuzi wapo tayari kutenda haki

Tuesday , 7th Aug , 2018

Kuelekea mchezo wa kesho Jumatano Agosti 11 wa game 3 ya 'best of three' nusu fainali ya michuano ya Kikapu ya Sprite Bball Kings kati ya Portland dhidi ya Mchenga Bball Stars, Kamishna wa ufundi wa TBF Manase Zabroni amesema waamuzi wamejipanga kuhakikisha haki inatendeka.

Waamuzi wa Kikapu wakiongozwa na Manase Zabroni (kulia).

''Kama tulivyoanza mwanzo wa mashindano kumekuwa hakuna lawama kuhusu waamuzi hivyo tutamaliza nusu fainali kesho kwa mwendo huo na mshindi atapatikana kwa haki na atakwenda kucheza fainali na wenzao wa Flying Dribblers ambao nao wamefika hatua hiyo bila malalamiko kwa waamuzi'' - amesema.

Mchezo wa kesho utazikutanisha timu za Portland dhidi ya Mabingwa watetezi wa michuano hiyo inayoandaliwa na East Africa Television LTD na kudhaminiwa na kinywaji cha Sprite, Mchenga Bball Stars. Mchezo huo ambao umekuja baada ya timu hizo kushinda mechi moja kila timu kwenye game 1 na game 2, utapigwa kwenye viwanja Don Bosco Oysterbay.

Mchenga Bball Stars (nyeupe) na Portland (kijani) kweye mechi ya game 2.

Portland walitoka nyuma kwa kupoteza game 1 kwa pointi 70 kwa 54 kabla ya kusawazisha game 2 kwa kushinda pointi 71 kwa 64. Game 3 itakuwa na ushindani mkubwa hususani kwa vinara wa pointi katika timu hiyo ambao ni Denis Babu kwa Portland mwenye pointi 104 kwenye mechi 5 na Baraka Sadick wa Mchenga mwenye pointi 64 katika mechi 4.

Mechi hiyo itakayotoa tiketi ya kwenda kucheza fainali na Flying Dribblers kuwania milioni 10 kwa bingwa, milioni 3 kwa timu itakayoshika nafasi ya pili na milioni 2 kwa MVP itaanza majira ya saa 10:00 jioni.
 

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini