Thursday , 20th Oct , 2022

Wafanyabiashara katika mji mkuu wa Ghana , Accra,wameanza mgomo wa siku kadhaa kwa kufunga biashara zao wakipinga hali mbaya ya uchumi nchini humo.  

Fedha ya Ghana imeshuka thamani kwa kasi kubwa mwaka huu huku mfumuko wa bei ukifikia 37% .

Serikali ya Rais Nana Akufo-Addo imekua ikitoa sababu zinazopelekea hali hiyo kuwa ni vita vinavyoendelea nchini Ukraine na janga la UVIKO 19. 

Jumatatu ya wiki hii wahadhiri wa vyuo vikuu nchini humo waligoma , wakishinikiza kulipwa posho zao. .