
Joseph ameuwawa kwa kukatwa panga na watu wasiojulikana kwenye mkono wake wa kulia usiku wa kuamkia leo Novemba 3/2022 akiwa nyumbani kwakwe.
Inaelezwa kuwa watu hao ambao idadi yao bado haijafahamika walivamia nyumba aliyokuwa akiishi Joseph Mathias na familia yake na kisha kutekeleza mauaji hayo
Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu mkoa wa Mwanza Alfred Kapole amesikitishwa na tukio hilo na kuiomba jamiii kuacha kufanya vitendo vya kikatili
kwa upande wake Kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Mwanza Mairi Makori amesema hadi Sasa tayari wanawashikilia watu watatu katika tukio hilo.