Wednesday , 21st Dec , 2022

Wanandoa wawili ambao wamefunga ndoa Desemba 17, 2022, wamefariki dunia jana Desemba 20, kwa ajali ya gari baada ya kulivaa kwa mbele basi la kampuni ya Luwinzo lililokuwa likitokea Ubaruku mkoani Mbeya kuelekea Dar es Salaam, katika eneo la Tanangozi mkoani Iringa.

Wanandoa waliofariki dunia

Wanandoa hao wote walikuwa ni watumishi wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha, na walifariki dunia wakiwa njiani kuelekea jijini Mbeya kwenye msiba na juhudi za kumtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa zinaendelea.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa Allan Bukumbi, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema ilisababisha vifo vya watu watatu na majeruhi wawili ambao wanapatiwa matibabu katika hospitali mkoani humo.