
Picha ya Angel Shakinyao (33)
Mkuu wa mkoa wa Songwe Waziri Kindamba, ameliagiza jeshi la polisi mkoani humo kuwasaka na kuwakamata watu wote waliohusika katika mauaji hayo.
Akitoa salamu za pole Mkuu wa mkoa wa Songwe Waziri Kindamba, amewataka wananchi kuwa na utulivu wakati jeshi la polisi likiendelea na uchunguzi.
Mwili wa Angel umeagwa katika makazi yake mjini Vwawa na kusafirishwa kwenda mkoani Dodoma kisha kupelekwa nyumbani kwao shinyanga kwa ajili ya mazishi.