Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwanafunzi mmoja afariki ajalini

Thursday , 30th Mar , 2023

Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Nyamilama Fadhili Maghembe,   amefariki dunia huku wanafunzi wengine 17 wakijeruhiwa kwenye ajali ya gari iliyotokea majira ya asubuh katika eneo la Gatuli kata ya Ng’undi wilayani Kwimba mkoani Mwanza.

 

Chanzo cha ajali hiyo kikitajwa kuwa ni mwendo kasi wa dereva ambapo gari hilo lilikuwa na wanafunzi 40 waliokuwa wakielekea Mwanza mjini kwa ajili ya likizo baada ya kufunga shule.

Mmoja wa wanafunzi waliokuwa katika gari hilo amesema gari lilimshinda dereva wakati akijaribu kukata kona baada ya kugonga bonde lililosababisha gari likose muelekeo na kwamba dereva huyo alikuwa mkaidi hata walipomsisitiza apunguze mwendo. 

Mganga mfawidhi wa hospitali  ya wilaya ya Kwimba Dk. Neema Gervas, amesema amepokea majeruhi 17 kwenye ajali hiyo huku mmoja akiwa amefariki dunia, na 12 kati yao wamepata majeraha makubwa huku wanafunzi wengine 6 wanafanyiwa uchunguzi wa mionzi .

"Wanafunzi 6 wamekwenda kwenye uchunguzi wa mionzi kwa sasa tunasubiri majibu ya X ray ili tuweze kujua hatua inayofuata pamoja na hapo tumeshatoa huduma ya awali ya dawa za maumivu na dawa za kuzuia tetenasi kwa wale wenye majeraha".

Mkuu wa wilaya ya Kwimba Ng’wilabuzu Ludigija, amefika katika hospitali ya wilaya ya Kwimba kuwajulia hali majeruhi wa ajaili hiyo na kutoa wito kwa madereva wote kuzingatia sheria za usalama barabarani kwa kuendesha gari kwa mwendo wa kawaida utakaomsaidia dereva kulimudu vizuri hata inapotokea dharura.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita