Taasisi za umma zaagizwa kutumia mfumo wa TANePS
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha kuwa taasisi zote za umma zinatumia Mfumo wa Ununuzi kwa Njia ya Mtandao (TANePS) na hatua kali zichukuliwe dhidi ya maafisa masuuli ambao taasisi zao zitakaidi matumizi ya mifumo katika ununuzi wa umma.