RC Mbeya adai vijana 150 kuvuruga uchaguzi
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, amesema serikali ya mkoa huo imejipanga kukabiliana na vijana 150 walioandaliwa kila Kata na vyama vya upinzani kwa ajili ya kufanya vurugu kwenye vituo vya kupigia kura siku ya Oktoba 28,2020, wakati wa uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani.