
Katibu wa kanisa la Anglikani Makambako Elias Ngailo amethibitisha kukutwa kwa mtu huyo, na kueleza kuwa amekutwa akiwa mtupu na amelala, hivyo wamelazimika kumsaidia kumvalisha nguo na kumpeleka kituo cha polisi wilaya ya kipolisi Makambako
Aidha katibu huyo amesema hajafahamu bado kama mtu huyo anajihusisha na imani za kishirikina au ana matatizo ya akili na kueleza kuwa pindi matukio hayo yanapotokea jamii haipaswi kujichukulia sheria mkononi
Naye Mwinjilisti wa kanisa hilo John Kisogo amesema mara baada ya kumkuta mtu huyo katika madhabahu hiyo wamelazimika kumfanyia huduma ya maombi na kufanya naye mahojiano ambapo hajui amefikaje kanisani hapo.
Hata hivyo mtunza hazina wa kanisa hilo Christopher Mtweve amesema kuwa huenda mtu huyo akawa na matatizo ya akili