
Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. George Simbachawene
Kauli hiyo ameitoa hii leo Desemba 27, 2021, baada ya taarifa mitandaoni zikieleza kuhusu tuhuma alizozitoa Askofu Mwingira kuhusu masuala ya mali zake na kunusurika kuuawa mara tatu.
"Tamko la Askofu Mwingira na mimi nimelisikia kwenye mitandao ni tuhuma nzito sana, kama haya matukio ni ndivyo yalitokea kwanini alikuwa hatoi taarifa polisi ili wahusika watafutwe, na yote yatokee wewe uko salama tu na baadaye unangojea mwisho wa mwaka na unasukuma lawama, kama aliyoyasema ni kweli tutahitaji atusaidie kutupa taarifa zaidi,”amesema Waziri Simbachawene.