Mfalme Zumaridi
Wakili wa serikali Emmanuel Luvinga, ameiambia Mahakama hiyo kuwa Zumaridi na wafuasi wake wapo tayari kupokea uamuzi huo wa Mahakama, ndipo Hakimu Mkazi Mfawidhi Monica Ndyekobora, akaiambia Mahakama hiyo kuwa kutokana na sababu zilizowasilishwa na mawakili wa upande wa utetezi kutokuwa na mashiko haoni haja ya kutoendelea na kesi hiyo.
Baada ya uamuzi huo wa Makahama, mawakili wa upande wa utetezi ulioongozwa na Steven Kitale, ukasema hawataweza kuendelea na shtaka hilo kutokana na matakwa ya kisheria na kuomba kupangiwa tarehe nyingine ili waweze kuwasilisha sababu zao za kutokuwa na imani na Hakimu huyo.