
Mwendesha mashtaka mkuu wa Peru amesema maafisa hao wanachunguzwa kwa tuhuma za mauaji ya halaiki, mauaji yaliyosababisha madhara makubwa
Ghasia hizo zilizuka baada ya aliyekuwa Rais Pedro Castillo kukamatwa mwezi Desemba mwaka jana kwa kujaribu kulivunja Bunge
Siku ya Jumatatu, watu 17 walikufa katika mapigano kati ya wafuasi wa Castillo na vikosi vya usalama kusini-mashariki mwa Peru huku wengine kadhaa wakijeruhiwa