Bright na Vanessa Mdee
Bright Music ameileza EATV & EA Radio Digital sababu za kuwa single ni,
"Siko kabisa katika mahusiano nawaangalia wenye maendeleo, wanawake hawawezi kuwa na 'lofa' lazima uwe na mchele 'pesa' pia uangalie hali yako".
Bright ameendelea kusema alikuwa kwenye mahusiano ila umaarufu umesababisha kuna vitu vingi vinatokea, wengi aliokuwa nao waliangalia nafasi yake na hakukuwa na mahaba.
Aidha Bright Music amesema kitu anachovutiwa kwa Vanessa Mdee ni mwanamke mzuri ambaye kila Mwanaume rijali lazima amuelewe na hisia zake zipo kwa Vanessa anampenda na anamkubali.
Bright ameendelea kusema kuwa jambo la kumpata Vanessa Mdee linaweza likawa hivi karibuni waombe uzima na kwa mahaba ambayo atampa atamtuliza mwenyewe.